Kwa kuwa miili yetu ilifanywa kuwa mahali ambapo Roho Mtakatifu (Yesu Kristo) ataketi na kukaa nasi katika kutuelekeza namna ya kuenenda katika uhalisia wa Neno, Tusome maandiko; 1 Wakorintho 6:20 19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; 20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu. Kama mkristo halisi unatakiwa utambue ya kuwa wewe ni hekalu la Roho mtakatifu maana tulikwisha kukombolewa na sisi si Mali yetu wenyewe yaani hatuwezi kujimiliki kwasababu yupo aliye mkuu kuliko sisi ambaye ndie anayetumiliki sisi (Bwana Yesu Kristo), na dhahiri ya kwamba tunajua ya kuwa Roho mtakatifu hafungamani na dhambi sasa Ikiwa unajiita mkristo alafu umeshindwa kufanya mwili wako kuwa hekalu la Roho mtakatifu kwa kujitunza kulingana na Neno, na kuepuka maovu yatokanayo na miili hii, bila shaka shetani ataufanya huo mwili utumike kama anavyotaka yeye maana ukisha mkataa R...
1 Petro 2:11-12 Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho. Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.